HIVI NDIVYO SIMU YAKO INAVYOWAFAHAMISHA WENGINE JUU YA MAHALI ULIPO

Miongoni mwa mambo ambayo simu yako ya kisasa  inaweza kuyafanya ni kukufahamisha ilipo kuliko kompyuta yako ya mezani,kompyuta mpakato wakati mwingine hata tablet ambavyo wakati mwingine ni vigumu kuwa navyo muda wote,simu za kisasa inaweza kujumuisha eneo ilipo na data katika upatikanaji wa habari ama taarifa  mbalimbali.

Kama ilivyo katika masuala mbalimbali ya teknolojia za kidijitali uwezo huu wa simu una uzuri wake na ubaya wake.Watumiaji wa simu wamekuwa wakijiuliza kuhusu masuala ya faragha hasa linapokuja suala la kufahamu mtumiaji wa simu alipo katika usalama wake.
Pia watu wengine hawako makini nahawafahamu  ni teknojia  gani ya kutambua mahali walipo na hasa kutokana na ukweli kwamba kuna program tumishi nyingi ambazo huhitaji kuonesha mahali mtumiaji wa simu alipo.
1.GPS
Global Positioning Systeam ni mtambo wa satellite unaotambua na kuelekeza maeneo mbalimbali hapa duniani.Mtambo huu unaoendeshwa na Kitengo cha Ulinzi cha Serikali ya Marekani ulianza kutimiwa katika simu mwaka 1990.Teknolojia hii inafanyakazi masaa 24 kwa siku na inauhakika wa kutoa muda halisi wa umbali Fulani,umbali wa mahali kwenda mahali pengine pamoja na kutoa muda wa sehemu mbalimbali za dunia kwa wakati mmoja.
Teknolojia hii iliyopo katika simu za mikononi  inaweza kutumika kuonyesha kifaa kilipo,kitakapokwenda ama kilipo.
Baadhi ya serikali duniani zimetengeneza mifumo yake ya GPS,japo haziingiliani na ule wa awali kwa kweli vinasaidia sana katika kufahamu mahali ulipo.Warusi wanao unaitwa GLONASS na wachina wanayo ambayo mwaka 2012 ilikuwa katika majaribio,Ulaya wanayo inaitwa Galileo na Japani inaitwa Quasi-Zeneth.
Mwaka 2012 Watalaamu wa kuunda wa simu za mkononi walikuwa katika mkakati wa kutengeneza processor ya simu ambayo itakuwa na uwezo wa kutumika katika aina zote za mifumo hii ya kufahama mahali ulipo.
2. Cell ID
 Pamoja na kuwepo kwa teknolojia ya GPS,Makampuni ya kutoa huduma za simu kwa maana ya mitandao ya simu yanafahamu eneo na mahali simu ilipo bila hata ya GPS,na walifahamu hili hata kabla simu hazijawekewa technolojia hii
Makampuni yanafahamu ni simu ya aina gani mteja anaitumia na umbali gani uliopo kati ya simu na simu nyingine kutokana na teknolojia iitwayo Cell ID ama kitambulisho cha simu,ambapo miongoni mwa vitu vinavyosaidia kufanyakazi kwa teknolojia hii ni minara ya simu. 
3.WI-FI
Wi-Fi inaweza kufanya vyema kwa namna teknolojia ya Cell ID inavyofanyakazi ,japo si kwa uwezo mkubwa sana kwa kuwa teknolojia ya Wi-Fi ina uwezo wa kufanya kazi katika eneo dogo ambapo ni sawa na mita 100.
Teknolojia hii hutumia njia mbili ya kwanza ni ile inayowezesha kuonesha kidokezo cha  uwezo wa kupokea masafa ya mawasiliano (RSSI) kwa kutumia masafa ya simu husika kwenye mtandao wa Wi-Fi
Njia ya pili inayotumika katika Wi-Fi ni utumiaji wa alama za vidole ambapo inaelezwa ni njema kwa mtumiaji wa ambaye anapenda kutembelea  eneo fulani mara kwa mara
Alama hizo za vidole zinaweza kutambua mahali ulipo kwa umbali wa mita chache.
4. Bluetooth
Naam utambuzi wa mahali unaweza kufahamika kwenye eneo husika  katika maduka yanayotumia kifaa cha kufahamu na kutunza kumbumbu bei za bidhaa kiitwacho beacons ambacho hutumia teknolojia ya Bluetooth,vifaa hivyo vinaweza kuwasiliana na simu ya mkononi yenye teknolojia ya Bluetooth 4.0.
Hizi ni baadhi tu ya teknojia zilizopo katika simu za kisasa ambazo zaweza kutumika kufahamu simu ilipo na hii inamaanisha kuwa simu ikifahamika ilipo basi hata mtumiaji wa simu hiyo naye anajulikana alipo kumbuka  kadri teknolojia inavyotuweka karibu unaweza kukimbia lakini huwezi kujificha

Chanzo: Maisha na Teknolojia

Geofrey Mtatiro

I'm a storyteller by trade but a problem-solver by birth. I find creative ways to tell stories of Individuals, Brands, Businesses & Organizations through Photography, Film Production & Advertising. In 2012, I founded BRAINBONGO to do just that while still in high school with the help of a few friends. Through the years, we have become really good at it. We love it and we live it. We are #EXTRAORDINARY!

Post a Comment

If you like this post be sure to leave a comment and share it with your friends. It will make my day!

Previous Post Next Post

Contact Form